Kilio cha watanzania hususani wakazi wa jiji la Dar ni kero ya upatikaji Majisafi na Salama kwa matumizi mbalimbali. Kumekuwa na sababu nyingi zinazochangia wananchi kutopata Maji hayo ikiwemo sababu ya uharibifu wa Miundombinu kwa wananchi wasiokuwa waaminifu kwa kukata mabomba na kujiunganishia Maji kiholela.

Kiwango cha Maji kinachopotea kwa mujibu wa DAWASCO ni kwa asilimia 54 ambapo kiwango hicho ni kikubwa zaidi kutoka kile cha kimataifa cha asilimia 16 kinachotakiwa.

Ofisa uhusiano wa DAWASCO, Bi Everlasting Lyaro (pichani) akiongea na waandishi mapema wiki hii alibainisha kuwa shirika limejipanga kwamba ifikapo 2020 kiwango cha Maji kinachopotea kiwe hakitozidi asilimia 25 ili kuwawezesha wananchi wengine kupata huduma hiyo.


“ipo mikakati mingi na mizuri ya kuhakikisha maji hayapotei ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa viongozi wa wananchi tukianzia kwenye ngazi ya Madiwani na watendaji wa serikali za mitaa ili waweze kuwaelimisha wananchi juu ya udhibiti upotevu wa Maji” alisema Lyaro.


Alisema 2015/2016 imeweka mikakati madhubuti na pia imejipanga kuhakikisha wizi wa maji unapungua ili kurudisha huduma hiyo kwa wananchi ambao wameikosa kutokana na hujuma ya wananchi wachache.

“Hivyo basi kutokana na kwamba tayari tumewabaini watu wanaofanya vitendo hivyo mwaka huu tumejipanga kuingia mtaani zaidi na kuhakikisha tunazungukia maeneo yote na tunapogundua kuwepo kwa tatizo hilo tunawachukulia hatua za kisheria” aliongeza Lyaro.

Wito kwa wananchi ni kushirikiana na DAWASCO katika kutoa taarifa za mara kwa mara pindi uhujumu wa miundo mbinu ya Maji na wizi wa Maji unapofanyika ili kujenga jamii yenye upatikanaji wa huduma hii kwa usawa na haki kwani maji ni Uhai.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...