Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiongoza matembezi ya Siku ya Kilele cha Mazoezi ya Viungo Kitaifa akiwa na Viongozi wengine yaliyoanzia katika Uwanja wa Tumbaku hadi Uwanja wa Amaan Studium leo asubuhi ambapo yamejumuisha Vikundi mbali mbali vya Unguja na Pemba.
Miongoni mwa vikundi vilivyoshiriki katika matembezi ya Siku ya Kilele cha Mazoezi ya Viungo Kitaifa ni kikundi cha KVZ Fitness Group kikiwa katika hali ya ukakamavu na nidhamu ya juu wakipita katika barabara Kariakoo kuelekea Komba wapya ambapo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein aliyaongoza matembezi hayo leo asubuhi.
Kundi la Mazoezi Zoni C wakiwa na bango lao linalosomeka "Siku ya Mazoezi Kitaifa 01Jan 2015 Mazoezi ni Tiba Mbadala",kama wanavyoonekanwa wakiwa katika matembezi ya Siku ya Kilele cha Mazoezi ya Viungo Kitaifa leo yaliyoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...