KIKOSI cha timu ya Friends Rangers, kesho kinajitupa kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam kuvaana na timu ya African Lyon, katika mchezo wa ligi daraja la kwanza. 
Ofisa habari wa Friends Rangers, Asha Kigundula, alisema kuwa mchezo huo wa pili kwa timu hizo ikiwa ni mzunguko wa pili wa ligi hiyo. 
 Kigundula alisema kuwa kikosi chao kipo katika hali kubwa ya kuhakikisha haitapoteza mchezo huo. 
 Alisema kikosi chao chini ya kocha wao Ally Yusuph 'Tigana' kina matumaini ya kufanya vizuri katika mchezo huo. 
 Kigundula alisema licha ya kutambua ugumu wa mchezo huo, lakini wana matumaini ya kufanya vizuri. 
 Alisema endapo watafungwa au kutoka sare timu yao itakuwa imepoteza mwerekeo wa kupanda daraja. 
 "Mchezo huo ni lazima tushinde; tusiposhinda tutakuwa tumejiweka pabaya zaidi katika kupanda ligi kuu msimu ujao"alisema Kigundula. 
 Rangers inashika nafasi ya nne ya msimamo wa ligi daraja la kwanza baada ya kupoteza mechi yake dhidi ya Lipuli, kwa kufungwa bao 1-0, kwenye Uwanja wa Samora Mkoani Iringa.
 African Lyon
Friends Ranger

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...