Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), linatoa taarifa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete atazindua nyumba mpya za makazi ya Wanajeshi eneo la Gongolamboto mnamo tarehe 10 Januari, 2015,    Saa 3:00 Asubuhi.
 
Aidha, uzinduzi wa nyumba hizo ni sehemu ya nyumba elfu kumi za  mwanzo za makazi ya Maafisa na Askari wa JWTZ zilizojengwa katika mikoa mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kuondoa tatizo la nyumba za makazi kwa Wanajeshi.
 
Ujenzi wa nyumba hizo za kisasa umefanywa na Kampuni iitwayo ‘Shanghai Construction Group’ ya Jamhuri ya watu wa China.
 
Waandishi wa Habari wanaombwa kuhudhuria na kufanya ‘Coverage’ katika tukio hili muhimu.
   
 
Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na  Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P  9203,   Dar es Salaam,  Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...