Na Faustine Ruta, Mwanza
Timu ya Wanawake kutoka Mkoa wa Kagera imetupwa nje ya Mashindano kwa Matuta baada ya kumaliza mtanange wao kwa sare ya Nyumbani ya Ushindi wa 2-1 na  Ugenini,CCM Kirumba Mwanza na Matuta kupigwa na Timu ya Mwanza kuibuka na Ushindi wa bao 4-3. 



Mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa CCM Kirumba Timu ya Mwanza ndio walianza kupata bao mapema dakika ya 2 kupitia kwa mchezaji wao matata Meriam Kimbuya (10) kwa kukatiza katikati ya mabeki na kufunga bao hilo la kwanza. Kipindi cha pili mchezaji huyo huyo Meriam Kimbuya aliwafungia bao tena Mwanza katika dakika ya 64 na kufanya 2-0 dhidi ya timu ya Kagera. Kagera waliongeza Bidii na dakika ya 73 Mchezaji Anna Katunzi aliachia shuti kali lililomzidi nguvu kipa wa Mwanza na kuishilia nyavuni na kufanya 2-1.
Kwenye kasi...... Mchezaji wa Kagera akiambaa na mpira
Kipa wa timu ya Mwana akiwapanga Wachezaji wakati wa kupiga mpira wa adhabu langoni mwake kipindi cha Kwanza. 
Nani zaidi!! Mahesabu ya kumtoka Mtu yanatakiwa hapa!!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...