Katibu Mkuu wa CCM,Abdulrahman Kinana pamoja na wanachama wa CCM wakiwemo na Wananchi kwa pamoja wakishiriki katika shughuli ya za uchimbaji na utandazaji wa mabomba ya mradi wa maji safi na salama katika shehia ya Kilimani,kwenye jimbo la Mjimkongwe.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipata maelezo mafupi ndani ya chumba cha kufundishia Kompyuta katika kituo cha Vijana (Tanzania Youth Icon),cha kuwaendeleza na kuwawezesha katika masuala mbalimbali ikiwemo elimu,Ajira na Michezo kilichopo Shehia ya Miembeni,Mwembemadema katika jimbo la Kikwajuni.
 Mwenyekiti wa Kituo cha Tanzania Youth Icon (TAYI),Bwan.Abdullah Miraji Othman akisoma hotuba Mbele ya Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kuhusiana na mambo mbalimbali yahusuyo kituo hicho cha huduma rafiki kwa Vijana kilichopo Muembemadema ndani ya jimbo la Kikwajuni sambamba na changamoto wazipatazo juu ya kituo hicho.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana  akizungumza mbele ya wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi nje ya Kituo cha Tanzania Youth Icon (TAYI),ambapo mlezi na mhamasishaji wake ni Mbunge wa jimbo la Kikwajuni,Mh.Hamad Yusuf Masauni.Kituo hicho cha TAYI ni Taasisi ya vyama visivyokuwa vya kiserikali,ambayo ina muelekeo wa kuwasaidiana na Wadau mbalimbali katika kufanikisha shughuli za maendeleo.Mwenyekiti wa Kituo cha Tanzania Youth Icon (TAYI),Bwan.Abdullah Miraji Othman amesema kuwa Taasisi hiyo hivi sasa ina ina wanachama wasiopungua 500 ambao tayari wameandikishwa na kuwepo katika rekodi na kumbukumbu za ofisi,Bwana Abdullah aliongeza kuwa kituo hicho kinawajenga vijana kiuchumi na pia kuwapa taaluma ya uongozi ili waje kuwa viongozi wazuri ,''kituo hiki kimekuwa kiwanda kizuri cha kuzalisha vijana wazuri kwa Taifa'',alisema Bwan.Abdullah .
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisalimiana na Balozi Ali Karume alipowasili katika Shehia ya Miembeni,katika jimbo la Kikwajuni,ambapo Ndugu Kinana alipokea taarifa fupi ya mradi wa Zahanati  na kushiriki katika ujenzi wa Taifa wa Ukarabati wa Zahanati ya Miembeni (Nyumba ya Yasu).Pichani kulia ni Muwakilishi wa jimbo la Kikwajuni,Mh.Mahamoud Mohamed Mussa pamoja na Mbunge wa jimbo hilo la Kikwajuni Mh.HamadiYussuf Massauni
Katibu wa NEC-Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akifurahia jambo na  Balozi Ali Karume  walipokutana leo katika Shehia ya Miembeni,katika jimbo la Kikwajuni.
Mmoja wa Mabalozi akifurahi mara baada ya kukabidhiwa baiskeli yake na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kwa shughuli mbalimbali za kichama,baiskeli hizo ilikuwa ni ni moja ya ahadi alizoahidi kutoa Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni,Mh Masauni,ambapo pia alitoa piki piki kwa makatibu wa chama. PICHA NA MICHUZI JR-ZANZIBAR

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...