
Na Bashir Yakub
Makala zilizopita nilieleza mambo au taarifa muhimu zinazopaswa kuwa kwenye mkataba wako unapokuwa unanunua nyumba/kiwanja. Nikasema katika niliyosema kuwa mkataba lazima uoneshe ukitokea mgogoro utatatuliwa vipi, ueleze kuwa utapotokea mgogoro muuzaji lazima awajibike kuhakikisha anakupa ushirikiano mnunuzi ili kumaliza mgogoro huo na kuwa muuzaji kama ana mke basi mke wake ni lazima aandaiiwe nyaraka iitwayo ridhaa ya mwanandoa ambayo ni tofauti na mkataba na aisaini pamoja na kuweka picha yake. Nilieleza mengi lakini hayo ni baadhi tu.
Kwa wale ambao hawakubahatika kuyasoma hayo basi waandike neno MAKALA SHERIA kwenye google watapata makala hizo. Leo tena naeleza hatua muhimu sana au ya lazima na lazima haswaa kwa mnunuzi wa kiwanja/nyumba ambayo anatakiwa apitie kabla ya kufanya manunuzi.Hatua hii kwa jina la kitaalam huitwa OFFICIAL SEARCH kwa lugha rahisi tu waweza kuiita utafiti,upekuzi, upembuzi au upelelezi rasmi ambayo hufanywa na wanasheria. Mi napenda niite upelelezi.
( 1 ) AINA ZA VIWANJA/NYUMBA UNAPOTAKA KUFANYA UPELELEZI KUJUA KAMA KUNA MGOGORO.
Nyumba/viwanja tunavyouziana kila siku vimegawanyika katika hadhi mbalimbali. Kwanza kuna nyumba/viwanja vyenye hati, vyenye leseni za makazi, vyenye ofa na ambavyo havina hati, leseni ya makazi wala ofa.
Kutokana na makuzi ya miji yetu viwanja/nyumba zenye hati mara nyingi huwa ni chache sana.Zenye leseni za makazi ni nyingi kiasi na haya ni maeneo ambayo hasa hujulikana kama uswahilini. Zenye ofa huwa ni chache nazo kwakuwa ofa ni hatua anayopitia mtu anapoelekea kupata hati au leseni ya makazi.
Matatizo mengine hutokana na kuwepo kwa kutokubaliana kati ya wale wanaouza ardhi hasa ndugu wakati mwenye ardhi anapokuwa amefariki. Migogoro hii ni mingi.
ReplyDelete