Na   Bashir   Yakub

Makala zilizopita  nilieleza   mambo au taarifa muhimu  zinazopaswa kuwa kwenye  mkataba wako  unapokuwa unanunua  nyumba/kiwanja. Nikasema  katika niliyosema  kuwa mkataba  lazima uoneshe  ukitokea mgogoro  utatatuliwa vipi,  ueleze kuwa  utapotokea mgogoro  muuzaji  lazima  awajibike kuhakikisha anakupa ushirikiano  mnunuzi  ili kumaliza  mgogoro huo na kuwa muuzaji  kama ana  mke  basi  mke wake ni lazima  aandaiiwe  nyaraka iitwayo  ridhaa ya mwanandoa ambayo  ni  tofauti  na mkataba  na  aisaini  pamoja na kuweka picha yake.  Nilieleza  mengi  lakini hayo ni baadhi tu. 

Kwa wale ambao  hawakubahatika kuyasoma hayo basi  waandike neno MAKALA  SHERIA  kwenye google watapata makala  hizo. Leo  tena naeleza hatua  muhimu sana au ya lazima  na lazima haswaa  kwa mnunuzi wa kiwanja/nyumba  ambayo anatakiwa  apitie  kabla ya kufanya manunuzi.Hatua hii kwa  jina la  kitaalam huitwa OFFICIAL  SEARCH  kwa lugha rahisi tu waweza kuiita  utafiti,upekuzi,  upembuzi au upelelezi rasmi  ambayo hufanywa na wanasheria. Mi napenda niite upelelezi.

( 1 )  AINA  ZA   VIWANJA/NYUMBA   UNAPOTAKA   KUFANYA  UPELELEZI  KUJUA   KAMA   KUNA  MGOGORO.

 Nyumba/viwanja   tunavyouziana  kila siku  vimegawanyika  katika hadhi mbalimbali. Kwanza  kuna nyumba/viwanja  vyenye hati, vyenye leseni za makazi, vyenye ofa na ambavyo havina hati, leseni ya makazi wala ofa.

Kutokana  na makuzi ya miji yetu  viwanja/nyumba zenye hati  mara nyingi huwa ni chache sana.Zenye leseni za makazi ni nyingi kiasi  na haya  ni maeneo ambayo  hasa hujulikana kama uswahilini. Zenye ofa  huwa  ni chache nazo  kwakuwa ofa ni hatua  anayopitia mtu anapoelekea  kupata hati au leseni ya makazi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Matatizo mengine hutokana na kuwepo kwa kutokubaliana kati ya wale wanaouza ardhi hasa ndugu wakati mwenye ardhi anapokuwa amefariki. Migogoro hii ni mingi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...