Mkurugenzi
wa Sensa na Takwimu,Ephraim Kwesigabo akizungumza na waandishi wa
habari hawapo nchini juu mfumuko wa bei kwa desemba mwaka jana.
Meneja
wa Utafiti wa Benki Kuu (BoT),Johnson Nyella akizungumza na waandishi
wa habari hawapo pichani juu ya sera za Benki Kuu katika kudhibiti
mfumuko.
Na Chalila
Kibuda na Globu ya Jamii,Dar.
Mfumuko wa
bei wa
Taifa wa Disemba 2014 ulipungua kwa asilimia 4.8 kutoka asilimia 5.8 Novemba mwaka jana. Akizungumza
na waandishi wa habari leo ofisini kwake Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu
Ephraim Kwesigabo alisema mfumuko wa bei kwa mwaka jana ulikuwa imara kutokana
uzalishaji mwingi wa vyakula.
Kwesigabo amesema
kasi ya upandaji wa bei na bidhaa na
huduma kwa mwaka jana imepungua kwa kasi
ikilinganishwa mwaka 2013 na fahirisi
za bei ziliongezeka disemba mwaka jana kwa kufikia 150.92 kutoka 144.07 mwaka
2013.
Aidha amesema
mfumuko wa bei wa mwezi Desemba,2014
unapimwa kwa kipimo cha mwezi umeongezeka kidogo kwa asilimia 0.2
ukilinganishwa na ongezeko la asilimia 0.6 mwezi Novemba,2014.
Hata hivyo amesema
kuwa mfumuko wa bei nchini una mwelekeo unaofanana na baadhi ya nchi nyingine za
Afrika Mashariki .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...