Familia ya Luteni Kanali Willy John Masoi (Mstaafu) wa Sabasaba Ukonga, Dar es Salaam tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa ndugu, jamaa, marafiki na majirani kwa msaada wa hali na mali wakati wa msiba wa Baba yetu mpendwa Luteni Kanali Willy John Masoi (Mstaafu) aliyefariki dunia Disemba 22, 2014 na kuzikwa Disemba 27, 2014 nyumbani kwake Dar es Salaam. 
Aidha shukrani za pekee tunatoa kwa Paroko, uongozi na walei wa Parokia ya Mt. Augustino ya Ukonga, Uongozi na wanajumuia wa Jumuia ya Mt. Monica ya Sabasaba Ukonga, Makamanda na Wapiganaji wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Uongozi na watumishi wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika (MAFC), Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Stadi (VETA), Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Tanzania (NAOT), Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi ya Dar es Salaam, Ofisi ya Umoja wa Mataifa New York. Tunatoa shukrani za pekee pia kwa Dk. Kaushik Ramaiya, madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Shree Hindu Mandal kwa huduma ya matibabu wakati wa uhai wa Baba yetu Mpendwa. 
Tunatambua pia michango ya kipekee ya wanaukoo wa Masoi na Minja, familia za Mshanga, Kajiru, Milanzi, Msolla, Msinjili, Leshabari, Mlay na majirani zao. 
“Raha ya milele umpe ee Bwana, na Mwanga wa milele umwangazie. Apumzike kwa amani”
Amina 
“Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo
 nimeumaliza, imani nimeilinda”

(2Tim 4:7)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Raha ya Milele Umpe Ee Bwana, na Mwanga wa Milele Umwangazie, Apumzike kwa amani. Amina.......Kristu........

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...