Na Bashir Yakub

Baada ya kuwapo tatizo hili wajibu mkubwa umebaki kwa watu wenyewe kuwa makini na waangalifu katika mununuzi ya ardhi. Ni uangalifu na umakini pekee ambao waweza kumsaidia mtu kuepukana na migogoro hii. Katika kuwa mwangalifu yapo mambo ambayo mtu anaweza kuyafanya . Moja ya mambo hayo ni kuwa makini kwa kuhakikisha unafuata taratibu zote unapokuwa unafanya mkataba wa manunuzi.
Mkataba wa manunuzi ya kiwanja, nyumba si jambo jepesi kama wengi wanavyolifikiria. Ni jambo nyeti hasa ikizingatiwa kuwa ardhi ni mali ya kudumu . Hii maana yake ni kuwa umri wote wa kiwanja au nyumba yako itakaoishi iwe miaka mia au mia mbili itakuwa inalindwa na mkataba huohuo.
Hakika si jambo jepesi. Nataka nieleze kuwa watu wengi wanafanya mikataba ya manunuzi ya viwanja nyumba kienyeji na kiholela. Wanafananisha mikataba hii na mikataba ya ununuzi wa vitu ambavyo haviishi hata miaka kumi kama magari.
Ni hatari sana na wengi wamepoteza nyumba na viwanja kimchezomchezo. Ubaya zaidi ni kuwa unapokuwa na mkataba wa kiwanja au nyumba ambao haukidhi viwango vya kisheria na bahati mbaya ukatokea mgogoro ni rahisi sana kupoteza eneo lako bila kujali ni kiasi gani umewekeza katika kulimiliki.
Darasa Tosha.
ReplyDeleteAhsante sana Mwanasheria wetu hapa na Mjomba Michuzi kwa kutufungua macho!