Na  Bashir   Yakub
Kwa muda mrefu sasa kumekuwepo na migogoro ya mashamba, viwanja na nyumba  hasa maeneo ya mijini.  Kwa utafiti wa kawaida utagundua kwa haraka baadhi ya sababu ambazo husababisha hali hii.Uaminifu, tamaa, kutelekeza maeneo kwa muda mrefu, utendaji mbovu wa  baadhi ya watumishi katika mamlaka za ardhi, uzembe na kutojali ni baadhi ya sababu  ambazo huchangia kuwapo  na kukua kwa tatizo hili. 

Baada ya kuwapo  tatizo hili wajibu mkubwa umebaki kwa watu wenyewe kuwa makini na waangalifu  katika mununuzi ya ardhi. Ni uangalifu na umakini pekee ambao waweza kumsaidia mtu kuepukana na  migogoro hii.  Katika kuwa mwangalifu yapo mambo ambayo mtu anaweza kuyafanya . Moja ya mambo hayo ni kuwa makini  kwa kuhakikisha unafuata taratibu zote unapokuwa unafanya mkataba wa manunuzi. 

Mkataba wa  manunuzi ya  kiwanja, nyumba si jambo jepesi kama wengi wanavyolifikiria. Ni jambo nyeti  hasa ikizingatiwa kuwa  ardhi ni mali ya kudumu . Hii maana yake ni kuwa umri wote wa kiwanja au nyumba yako  itakaoishi iwe miaka mia au mia mbili itakuwa inalindwa na mkataba huohuo. 
Hakika si jambo  jepesi. Nataka nieleze kuwa watu wengi wanafanya  mikataba ya manunuzi ya viwanja nyumba kienyeji na kiholela. Wanafananisha mikataba hii na mikataba ya ununuzi wa vitu ambavyo haviishi hata miaka kumi kama magari. 
Ni hatari sana na wengi wamepoteza nyumba  na viwanja kimchezomchezo. Ubaya zaidi ni kuwa unapokuwa na mkataba wa  kiwanja au nyumba ambao haukidhi viwango vya kisheria  na bahati mbaya ukatokea mgogoro ni rahisi sana kupoteza  eneo lako bila kujali ni kiasi gani  umewekeza katika kulimiliki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Darasa Tosha.

    Ahsante sana Mwanasheria wetu hapa na Mjomba Michuzi kwa kutufungua macho!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...