Na Andrew Chale
USIKU wa Old is Gold taarab  unatarajiwa kurindima ndani ya ukumbi wa Safari Carnival, Mikochezni B, kwa wadau kupata burudani ya muziki wa mwambao wa kizamani.
Kwa mujibu wa waandaji wa usiku huo, Mkurugenzi wa Fabak Fashions, Asia Idarous Khamsin alieleza kuwa  ni kila Jumapili  ndani ya ukumbi huo utakuwa na burudani ya kipekee kwa nyimbo za mwambao pamoja na ‘surprise’ mbalimbali kwa watakaofika hapo.
“Kila jumapili  kwa kiingilio cha sh 5,000 tu. Wapenzi wa muziki wa wambao  watashuhudia shoo ya Usiku wa Old is Gold ndani ya Safari Carnival” Alisema Asia Idarous.
Aliongeza kuwa, mbali na burudani ya taarab za zamani  pia kutakuwa na ‘Surprise’ mbalimbali" kwa wadau watakaojitokeza kwenye usiku huo.
Aidha,  Asia Idarous alisema usiku huo, pia umedhaminiwa na  Safari Carnival, Fabak fashions, Clouds
Fm, Gone Media, Maji Poa, Michuzi Media Group na wengineo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...