Makampuni mengi hapa jijini yamebuni utaratibu wa kuwatumia vijana wanaotembea kwa kutumia viatu vya matairi (Roller Skating) katika kusambaza ujumbe na matangazo yao mbali mbali,jambao hilo ni jema sana hasa ukizingatia kuwa sasa hivi swala la ajira ni changamoto.Vijana hawa hufanya kazi ya kugawa vipeperushi kwa wenye magari na watembea kwa miguu katika makutano makuu wa mabarabara hapa jijii Dar,kama walivyokuta na Kamera Mani wa Globu ya Jamii maeneo ya Magomeni Mapipa hivi karibuni.
Mmoja wa vijana hao akipiga misele barabarani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ni vizuri lakini ningeshauri au kupendekeza, vijana hao na hata hao waajiri wao, wazingatie suala zima la 'healthy and safety' kwa vijana hao, hili nikimaanisha uvaaji wa 'High Vis Jackets' ikiwezekana hata helmets, kwani kazi zao hizo na hizo 'roller skating' barabarani ni hatari zaidi na khasa kwa madereva wetu hawa wa kibongobongo wasiojali wala kuzingatia sheria za usalama barabarani, inakuwa ni hatari zaidi endapo hawatavaa reflective and protective equipment wawapo kazini. (Ni ushauri tu)

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...