Katibu wa Jumuiya ya Wafanyakazi wastaafu Pemba Bwana Majid Moh’d akimkabidhi risala Mkamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwenye hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini ya Jumuiya hiyo hapo ukumbi wa Tasaf Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Chake chake Pemba.
Baadhi ya Wajumbne wa Bodi ya Wadhamini ya Jumuiya ya Wafanyakazi Wastaafu Pemba akifutilia Hotuba ya Balozi Seif hayupo pichani wakati akiizindua rasmi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiizindua rasmi Bodi ya wadhamini ya Jumuiya ya Wafanyakazi Wastaafu Pemba hapo ukumbi wa Tasaf uliopo Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Chake chake Pemba. Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.

Wastaafu wa Taasisi za Umma za Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na zile za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wanapaswa  kushirikiana kwa karibu katika kutumia ujuzi na Taaluma zao za muda mrefu ndani ya Jumuiya wanazozianzisha baada ya kustaafu kwao  ili waendelee kuchangia Maendeleo ya Taifa.

Kauli hiyo imetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakati akiizindua rasmi Bodi ya wadhamini ya Jumuiya ya Wastaafu Pemba hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Tasaf  uliopo katika Majengo ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar yaliyopo Chake chake Pemba.

Balozi Seif alisema mashirikiano hayo yatatoa nafasi nzuri kwa wastaafu hao kuondoa shaka ya kuendeleza maisha yao kwani baadhi yao hupata wakati mgumu  kabla na baada ya kustaafu kwa vile wanakuwa bado hawajajipanga.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...