App inayoonyesha vivutio mbalimbali vya kitalii  nchini Tanzania,  App hiyo ambayo imeandaliwa na Bi. Benita Cassar Torreggiani kwa  kusaidiwa na wataalam kutoka Apple  inaweza kupatikana kupitia  mitandao ya Ipad, Iphone na  Smart Phone. 
 Mfanyakazi wa Apple Store Grand Centra jijini New  York ambako onyesho hilo lilifanyika akimtambulisha Bi. Benita.
 Balozi Tuvako Manongi Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika  Umoja wa Mataifa,  akizungumza  na Bi . Benita ambapo alimshukuru kwa uamuzi wake huo wa kutangaza utalii wa  Tanzania kupitia App hiyo.

Na  Mwandishi Maalum,  New  York
 Katika kuhakikisha kwamba taarifa   kuhusu   vivutio mbalimbali  vya kitalii vilivyopo nchini  Tanzania  zinawafikia watalii wengi  na kwa urahisi  nchini Marekani na kwingineko , jana  ( alhamis) palifanyika onyesho  la App  inayotoa huduma hiyo kupitia Ipad, Iphone na Smart Phones.
 App hiyo ijulikanayo kama  “ Official Destination Tanzania, Zanzibar, Serengeti, Ngorongoro and Kilimajaro”,  imeandaliwa  Bi. Benita Cassar Tirreggian akisaidiwa na wataalam kutoka kampuni ya Apple kupitia mpango wao ujulikanao kama one to one.
 Onyesho la App hiyo  ambalo lilikuwa   kivutio kwa wageni walioalikwa  akiwamo  Mwakilishi wa Kudumu wa   Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi, limefanyika katika duka linalouza  bidhaa za Apple ambalo lipo  katika Kituo Kikuu cha Treni ( Grand Central) jijini New York.
Baadhi ya washiriki kutoka TANAPA ambao wapo  hapa New York kushiriki onyesho jingine la masuala ya kitalii  maarufu kama New York Times  Travel Show nao walihudhulia onyesho la App hiyo.
Akielezea ni  kwa nini  aliamua kutengeneza App hiyo,  Bi. Benita aliwaeleza wageni waalikwa kwamba  mapenzi yake mkubwa  kwa  Tanzania  ndio hasa kulikochangia  yeye kuamua kuitengeneza App hiyo  ili uzuri wa nchi ya Tanzania, watu wake na  maliasili zake ushuhudiwe na kuwavutia watu wengi zaidi.
Akaongeza kuwa pamoja na utaalam na usaidizi kutoka Kampuni ya Apple,  Serikali ya Tanzania pamoja na wadau wa sekta ya utalii, walimpatia ushirikiano mkubwa katika   utengenezaji wa App hiyo ambayo anasema imeridhiwa na Serikali.
Balozi  Tuvako Manongi alimshukuru  Bi. Benita kwa uamuzi wake huo na pia akawashuru wageni mbalimbali waliohudhuria onyesho hilo huku akiwatia shime ya  kwenda Tanzania kujionea na kufurahia utajiri mkubwa wa maliasili kwa maana ya mbunga za wanyama,  bahari yenye kila aina ya vivutio na mengine mengi  ambayo Tanzania imebarikiwa kuwa nao.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Safi sana-nimesha i download and I can only recommend it :-)

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...