BENKI ya Exim imetoa wito kwa wateja wake kutumia vyema fursa ya ugunduzi uliopo katika sekta ya gesi  nchini kwani ina uwezo wa kubadilisha muundo wa uchumi uliopo na kujenga uchumi mpya uliojengeka katika utegemezi wa gesi asilia ambao utakua na matunda makubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya kibenki na biashara.

Wito huo ulitolewa na Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa benki hiyo, Bw. Dinesh Arora wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni maalum kwa ajili ya wateja wake wakubwa.

Zaidi ya hayo, Arora alieleza kuwa sekta ya gesi inaambatana na fursa nyingi ambazo zinaweza kutumiwa na wadau mbali mbali waliopo katika sekta binafsi. Alitaja maeneo yenye fursa kuwa ni pamoja na matengenezo ya vifaa, ujenzi, huduma za mazingira na Mafunzo ya Ufundi.

“Ni imani yetu kama benki ya Exim kuwa, katika siku zijazo, kutakuwa na ongezeko kubwa la mahitaji ya makazi, sehemu za burudani, utalii, elimu na huduma za afya. Jukumu kubwa la sekta binafsi itakuwa ni kukuza uhusiano na sekta ya gesi na kugundua na kuzitumia fursa,” alisema.

Akizungumzia juu ya ukuaji wa uchumi nchini, Arora alisema kuwa makampuni yanahitaji mipango na mikakati ya kifedha ya muda mrefu ili kuweza kufikia mahitaji na malengo yao ya ukuaji.

 “Kama benki ya tano kwa ukubwa Tanzania, Benki ya Exim inatoa huduma za kibenki za uwekezaji katika mfumo wa ushauri na ‘intermediary’ ili kuzalisha na kuongeza mtaji kwa njia ya ‘debt and equity’ kwa wateja wakubwa,” alisisitiza..

Arora aliendelea kuwaasa wateja kutumia kitengo cha benki hiyo cha huduma za kibenki za uwekezaji, ambacho kwa sasa kina huduma mpya zilizotengenezwa maalum ili kukidhi mahitaji mahsusi ya wateja wake, zikiwemo Project Financing, Debt na Equity Syndication services na Private Equity na M & A Advisory Services.

Arora alisema kuwa benki yake imejenga uwezo mzuri katika suala hilo na piaimeongeza nguvu zaidi katika muundo wake wa uongozi ili kusaidia katika kurahisisha uwepo wa uhusiano wa kimataifa na kuongeza  mtandao na wawekezaji. “Tumejiimarisha zaidi na tumefanya maombi ya vibali mbalimbali stahiki na pia tumeungana na wawekezaji,” alisema.  
  
Akizungumzia huduma zinazopatikana katika kitengo hicho cha huduma za kibenki za uwekezaji, Arora alisema moja ya huduma zinazotolewa na kitengo hicho ni pamoja na ushauri bora wa kimkakati kwa wateja wake.


“Muundo wa benki yetu unaturuhusu kuwahudumia wateja wetu na kuwapatia ufumbuzi wa mahitaji yao ya kimkakati na kifedha katika nyanja zote. Tunawiwa kuwa mshauri nambari moja kwa wateja wetu ikiwa ni pamoja na makampuni binafsi, taasisi za fedha, mamlaka za umma, wawekezaji na wakopeshaji,” alisema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...