Licha ya jitihada zinazoendelea kufanywa kuzuia uhujumu miundombinu ya Majisafi na wizi wa Maji, hujuma nyingine kubwa ya chuma chakavu za MAJITAKA imebainika baada ya DAWASCO kukamata mifuniko ya Majitaka katika kiwanda cha nondo cha IRON&STEEL cha jijini Dar es salaam.

 Vyuma Chakavu hivyo ambavyo ni mifuniko ya chemba za Majitaka za DAWASCO zimebainika baada ya uchunguzi wa kina na taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuhusu upatikanaji wa mifuniko hiyo kiwandani hapo.

Afisa Uhusiano wa DAWASCO Bi Everlasting Lyaro alisema ilibidi watumie mbinu mbadala ili kubaini biashara hiyo iliyokuwa ikiendelea kiwandani hapo, ambapo kwa kushirikiana na Polisi kutoka kituo cha kijitonyama na Afisa Mtendaji wa kata ya Mikocheni waliweza kuvamia kiwanda hicho na kukuta mifuniko mingi ya chemba za Majitaka ambazo ni mali ya DAWASCO.

“Bei ya mfuniko mmoja wa Majitaka huwa tunanunua kati ya Tsh laki tano hadi sita (500,000 -600,000) kutegemeana na ukubwa wa mfuniko, lakini hawa wakishaiba huwa wanaenda kuuza sh 500 kwa kilo hivyo unakuta gharama kubwa inabaki kwetu sisi tunaotoa huduma hii” alisema Lyaro

“mifuniko ya chemba za Majitaka ni muhimu kwa uhifadhi wa Majitaka na pia kuzuia uchafu huo kutapakaa ovyo mitaani, hivyo kuendelea kushamiri kwa biashara hiyo kunatupa wasiwasi wa uwezekano wa magonjwa ya mlipuko utakaosababishwa na utiririshwaji wa Majitaka ovyo mitaani” alifafanua Lyaro Aliongeza kwa kusema mapambano ya uhujumu katika miundombinu ya DAWASCO bado ni kubwa na inahitaji ushirikiano wa pamoja kati ya wananchi, viongozi husika pamoja na DAWASCO katika kulinda na kuhifadhi miundombinu ya Majisafi na Majitaka.

Katika tukio hilo Meneja Mkuu wa kiwanda hicho Raju N. Chita na Meneja utumishi Idrisa Ally wamekamatwa na kufikishwa kituo cha polisi kijitonyama na kufunguliwa Jalada namba KJN/1786/2015 kwa hatua zaidi kisheria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. safi sanaaa...Nimefurahi sana...Japo nilikuwa naamini kuwa tu hili suala Viongozi wanalifungia macho sababu walikuwa wanajua wazi wapi hii mifuniko ya maji taka inapelekwa...

    Mabarabarani Mifuniko hii inapotolewa imekuwa ikisababisha hata ajali wakati mwingine kutokana na mashimo yake kuwa wazi na kutojua usiku.

    Ningeomba Walipishwe mabilioni yatakayotosheleza kurudisha mifuniko yote ya majitaka iliyoibiwa Dar nzima...Shame on them

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...