Bendi ya muziki INAFRIKA BAND aka "Wazee wa Indege" kutoka jiji Dar es salaam, imelitingisha jiji la Bremen, nchini Ujerumani katika onyesho liliofanyika usiku wa 13 Februari 2015 katika ukumbi mkubwa wa Musik-Theater mjini humo. 
Bendi hiyo kutoka Chang'ombe ilisimama jukwaani na kuziteka nyoyo za maelfu ya wapenzi wa muziki kiasi cha kutajwa kuwa bendi bora ya muziki wa Folk na radio Funkhaus-Europe kutokana na vionjo vya mitindo ya muziki wa asili wa makabila ya Kitanzania vilivyotumiwa na Inafrika Band katika kuteka yonyo za washabiki kila kuona duniani.
 Inafrika Band, ambayo  imefanikiwa kuliweka jina la Tanzania katika tufe la dunia kwa kutumia mitindo yake ya vionjo vya kiasilia, inaongoza katika  kufanya tour ndefu duniani,
Hadi sasa  wameshafanya ziara katika mabara yote duniani kuanzia Afrika, Austalia, Amerika, Asia Ulaya na visiwa vya Karebiki. 
Wakali hawa wa mdundo inayokubalika kimataifa wanatisha na kuzoa washabiki kwa dhoruba kali la mtindo wao wa muziki. 
Inafrika band inatuwakilisha na hivi sasa bado wapo katika ziara ndefu ughaibuni kuhakikisha  kuwa muzikiwa wao unasikika kila kona nje ya mipaka ya Tanzania.
Usikose kuwasikiliza Inafrika Band "Wazee wa Indege" kupitia  http://www.inafrikaband.co.tz
Pia unaweza kuwapa  hi kupitia info@inafrikaband.co.tz ii
 INAFRIKA BAND aka "Wazee wa Indege" kutoka jiji Dar es salaam wakifanya onesho kubwa katika jiji la Bremen, nchini Ujerumani, usiku wa 13 Februari 2015 katika ukumbi mkubwa wa Musik-Theater jijini humo. 
Ngoma ya "Indege" ikivurumishwa
Kazi mbele kwa mbele
Nyomi ya mashabiki wa jiji la Bremen

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Wakubwa Inafrika Band basi tupieni pia video clips zenu YouTube kwa kufungua account.

    Maana vitu mnavyofanya ni vya uhakika sana.

    Mdau
    Muziki wa Kweli

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...