Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania, akisalimiana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Kanda ya Tabora, Mhe. Simba alipowasili MKOANI Tabora leo kwa ajili ya ziara ya kutembelea Mahakama mkoani humo.
Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania, akisalimiana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Bi. Suzan Kaganda alipowasili mapema Leo mkoani Tabora kwa ajili ya ziara.
Baadhi ya Watumishi wa Mahakama mkoani Tabora wakisubiri kumpokea Mhe. Jaji Mkuu .
Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania akipata Maelezo mafupi kutoka kwa Mhe. Amir Mruma, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu (aliyesimama) Kanda ya Tabora alipowasili katika jengo la Mahakama Kuu Kanda ya Tabora kuanza rasmi ziara yake ya kikazi. Wengine walioketi ni Waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Tabora. (Picha na Mary Gwera, Mahakama).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...