Mwigizaji  Julianne Moore ndiye mshindi wa mwaka huu wa waigizaji sinema wa kike na kushinda tuzo ya Oscar kwa kucheza vyema kwenye filamu ya "Still Alice."
Usiku wa kuamka leo huko Marekani, Moore amewashinda Felicity Jones ("The Theory of Everyting"), Marion Cotillard ("Two Days, One Night"), Reese Witherspoon ("Wild") na  Rosamund Pike ("Gone Girl) katika kinyang'anyiro hicho.  Awali alipendekezwa mara tano kugombea tuzo hiyo ya juu katika tasnia ya sinema duniani, na ni mmoja wa waigizaji 11 ambao wamewahi kupendekezwa kushindania tuzo hiyo mara mbili katika mwaka mmoja wa 2003, kwa umahiri wake katika filamu za  "Far From Heaven" na  "The Hours".  Hii ni mara ya kwanza kwa  Moore kushinda tuzo hiyo.

Kinyang'anyirko kikali cha ni mwigizaji gani wa kiume aliye bora kwa mwaka huu hatimaye kimepata mshindi usiku wa kuamkia leo huko Marekani, ambapo Eddie Redmayne amenyakua tuzo ya  Oscar na kuwa mwigizaji bora wa kiume kwa umahii alionesha katika filamu ya  "The Theory of Everything."
Redmayne aliwashinda kina Steve Carell ("Foxcatcher"), Bradley Cooper ("American Sniper"), Benedict Cumberbatch ("The Imitation Game") na  Michael Keaton ("Birdman") katika ngwe hiyo ambayo hata hivyo  Keaton ndiye aliyetoa upinzani mkali sana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Huyu Dada Julianne Moore namkubali sana, kwa wale wanao penda comedy, family movie anaweza sana. Inakipaji cha hali ya juu. sinema zake utazani za kweli.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...