Mkurugenzi
wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa Tamasha la Pasaka Bw. Alex
Msama akikabidhi vyakula mbalimbali kwa Halima Ramadhan Mlezi wa kituo
cha kulelea watoto yatima cha Mwandaliwa kilichopo Tegeta jijini Dar es
salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, ikiwa ni moja ya misaada inayotolewa
katika vituo mbalimbali vya kulelea watoto yatima wakati wa msimu huu
wa maadalizi ya Tamasha la Pasaka linalotimiza miaka 15 tangu
lianzishwe.
Msama
amekabidhi misaada hiyo kwa vituo vitano vya kulelea watoto waishio
katika mazingira magumu,makabidhiano ya misaada hiyo ilifanyika kwenye
ofisi za kampuni hiyo,Kinondoni jijini Dar.
Msama
alisema kuw maandalizi ya tamasha hili yanaendelea vyema mpaka sasa,na
kwamba tamasha hilo linatarajiwa kufanyika jijini Dar April 7
2105,ambapo litashirikisha waimbaji mbalimbali wa Kimataifa na wa
Nchini,aliongeza kuwa ili kunogesha zaidi tamasha hilo pia kutakuwepo na
michezo mbalimbali itakayochezwa ikiwemo na kukabidhi zawadi na vikombe
kwa washiriki wa tamasha hilo.
katika hatua nyingine Bwa.Alex Msama amelaani
matukio ya mauaji ya Albino hapa nchini,ameiomba Serikali kutilia mkazo
katika janga hilo ambalo limekuwa likiibua na kuzua gumzo miongoni mwa
jamii,hivyo ameiomba Serikali kuwashughulikia ipasavyo wahusika wote waliofanya na wanaofanya ukatili huo ambao ni kinyume kabisa na maadili ya nchi yetu,na ikibidi kukomesha kabisa matukio hayo ambayo yamekuwa yakilitia aibu Taifa letu.
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa Tamasha la Pasaka Bw. Alex
Msama akikabidhi vyakula mbalimbali kwa Honorata Michael Mlezi wa kituo
cha kulelea watoto yatima cha Honorata kilichopo Temeke jijini Dar es
salaam.
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa Tamasha la Pasaka Bw. Alex
Msama akikabidhi vyakula mbalimbali kwa Soud Said Mwakilishi wa kituo
cha kulelea watoto yatima cha Ijanzo Zanda orphanage Centre cha jijini
Dar es salaam
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...