BABA mzazi wa msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini, Dully Sykes, mzee Ebby Sykes amefariki dunia jioni ya leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa Presha.

Ebby Sykes alikuwa muimbaji na mpiga gitaa mashuhuri na ndiye anayedaiwa kumfundisha mambo mengi ya muziki mwanae Dully Sykes.

Sykes alizaliwa February 24, 1952 ambapo tarehe hiyo mwaka huu alikuwa anatimiza miaka 63.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

-Amen

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Inna Lillahi Wainna Ilay Rajiuun. Mwenyeez Mungu amjaaliye safari ya kheri, amughufiri kwa yote, amnusuru adhabudhe na amjaaliye palipo pema peponi - Ameen. Pole sana Dully, poleni wanafamilia wote na kila aliyekhusu ama kuguswa na msiba huu. Daima tukumbuke, duniani ni mapito na akhera marejeo na ndio khatamia yetu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...