MWIMBAJI mahiri wa  nyimbo za Injili nchini, Upendo Kilahiro amesema kuwa endapo atapata nafasi ya kushiriki kwenye miaka 15 ya Tamasha la Pasaka mwaka huu, ataimba nyimbo zilizopo katika albamu yake mpya inayotarajia kukamilika hivi karibuni.
 
Kwa mujibu wa Kilahiro tamasha hilo ni maalum kwa sababu  linatimiza miaka 15 tangu kuanzishwa kwake hivyo akipata nafasi katika tamasha hilo ataimba nyimbo mpya kama zawadi kwa watanzania.
 
Alipotakiwa kuitaja albamu hiyo na baadhi ya nyimbo zilizomo humo alisema ni mapema kuitaja hata hivyo nia yake ni kuwashitukiza watanzania watakaopata fursa ya kushiriki tamasha hilo ambalo litakuwa la aina yake.
 

Alisema iwapo atapata nafasi katika tamasha la mwaka huu ataimba nyimbo hizo mpya na zile za zamani ambazo zinatamba katika ulimwengu wa muziki wa injili huku akiwaomba watanzania kufika kwa wingi katika tamasha hilo litakuwa tofauti na mengine yaliyowahi kufanyika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...