Pichani kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari
wakati akielezea maendeleo ya maandalizi ya miaka 15 tangu kuanzishwa
kwa tamasha la Pasaka, sherehe ambazo zitafanyika wakati wa sikukuu ya
Pasaka jijini Dar es salaam na kisha mikoani, Akizungumza katika mkutano
huo Msama amesema mwaka huu tamasha la pasaka ni maalum kwa Msama
Promotion imepanga kuwanunulia baiskeli 100 za walemavu ambazo
zitagawanywa katika mikoa 10 hapa nchini.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akifafanua zaidi kwa waandishi wa habari kuhusiana na maandalizi ya miaka 15 tangu kuanzishwa
kwa tamasha la Pasaka, na pia sherehe hizo zitaambatana na utoaji wa baiskeli 100 za walemavu ambazo
zitagawanywa katika mikoa 10 hapa nchini.
Msama
ameongeza kuwa hivi sasa wako katika mazungumzo na waimbaji wa muziki
wa injili kutoka nje ya nchi hasa kule Afrika Kusini na Uingereza,
waimbaji ambao wako katika mazungumza na kampuni ya Msama Promotion ni
Solomon Mahlangu, Rebecca Malope, Keke Pofolo na wengine wote kutoka
nchini Afrika Kusini.
Msama alisema kuwa idadi ya mikoa ambayo imeomba iandae onesho la miaka 15 ya Tamasha la Pasaka sasa
imefikia 17,amesema Tamasha la Pasaka kwa mwaka huu litakuwa la aina yake tangu walipoanzisha tamasha lao mwaka 2000.
“Tumepokea
maombi ya wadau kutoka mikoa 17 wakitaka tupeleke Tamasha la Pasaka mikoani
kwao. Tunachofanya kwenye kamati yangu ni kupokea maoni kwa njia mbalimbali kwa
wadau wetu wa huko.
“Lakini si kupendekezwa au kuombwa tu na wadau
ndiyo kigezo cha kupewa nafasi, lazima tuangalie na mazingira ya mkoa husika
katika mambo ya matamasha,” alisema Msama.Aliitaja
mikoa hiyo kuwa ni Morogoro, Rukwa,
Mara, Singida, Arusha, Ruvuma, Mbeya, Iringa, Tanga, Dar s Salaam,
Mtwara, Mwanza, Dodoma, Tabora, Shinyanga, Kilimanjaro na Zanzibar.
Alisema
kamati yake inatarajia kukutana Jumatano wiki hii na kufanya tathmini ya maombi
kwa wadau wao wa maeneo hayo ili kupata mikoa sahihi ambayo tamasha hilo
litafanyika mwaka huu.
Tamasha
la Pasaka linaandaliwa na Kampuni ya Msama Promotion ya jijini Dar es Salaam,
ambayo pia huandaa Tamasha la Krismas kila mwaka, lakini wanataka Tamasha la
Pasaka mwaka huu liwe bora zaidi kwa sababu wanasherehekea miaka 15 tangu
waanzishe tamasha hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...