Meneja wa Mfuko wa Bima ya Afya Mkoa wa Kinondoni ,Grace Temba akizungumza leo na wajasirimali wa Mkoa wa Kinondoni (hawapo pichani) juu ya faida ya kujiunga na mfuko huo kupitia Mtandao wa ASEE iliyofanyika katika ukumbi Pricess ,Sinza Jijini Dar es Salaam.
 Afisa Matekelezo na Uratibu wa NHIF,Catherine Masingisa akitoa maada kwa wajasirimali wa Mkoa wa Kinondoni (hawapo pichani) namna ya kujiunga  na mfuko wa Bima ya Afya  kupitia vikundi vya ujasiriamali iliyofanyika Katika Ukumbi wa Princes ,Sinza jijini Dar es Salaam.
 Sehemu ya wajasiriamli wakisikiliza maada kutoka kwa maafisa wa NHIF katika ukumbi wa Princess ,Sinza jijini Dar es Salaam.Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii.
=======  ========  ======  =========
 Na Chalila Kibuda.

Mfuko wa taifa wa Bima ya Afya (NHIF)umewataka wajasiriamali wajiunge katika Mtandao wa Jamii wa Huduma ya Afya (ASEE)ili waweze kupata huduma ya afya kwa kuchangia Sh.78,600 kwa mwaka mzima.

Akizungumza na wajasiriamali wa Mkoa wa Kinondoni,Afisa Matekelezo na Uratibu ,Catherine Masingisa amesema si wakati wote mjasiriamali hawezi akawa fedha ya matibabu kujiunga na mfuko kunamfanya aweze kupata matibu katika vituo vyote vilivyosajiliwa na mfuko huo.

Masingisa amesema mpango huo wa kurasimisha wajasirimali kupitia mtandao unatambulika kama Kikoa kutokana na michango yao inakusanywa sehemu moja na kupelekwa katika mfuko wa NHIF.

Amesema watanzania wote wanatakiwa kuwa kadi ya mfuko wa bima ya afya ili kumuwezesha kila mtu kupata matibabu sehemu yeyote kutokana na hali ya uchumi,kwa sababu mtu hawezi kuwa na fedha wakati wote.


Kwa upande wa Afisa Mtekelezo na Uratibu,Tumaini Geofray amesema mfuko umejipanga kufikia wananchi wote juu ya kuwaelimisha faida ya kujiiunga na mfuko huo  kupitia vikundi ili kupata urahisi wa kuratibu zoezi hilo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...