Na Bashir Yakub

Kuomba talaka si dhambi. Kama lingekuwa dhambi sheria isingeruhusu jambo hilo kwakuwa si kawaida ya sheria  kuhamasisha madhambi.  Ni kwasababu hii nasema kuwa atakayeona amebanwa basi aombe talaka. Si kosa hata kidogo kufanya hivyo isipokuwa ndivyo tunavyoelekezwa  na sheria zetu tunazozipenda na kuziheshimu sana.

1.   KUVUNJIKA  KWA  NDOA.

Kuvunjika kwa ndoa kwa mujibu wa sheria zetu za Tanzania kuna mazingira mengi. Baadhi ya mazingira hayo ni yale yaliyoorodheshwa kifungu cha 12 (a-e) cha Sheria ya ndoa ambayo ni pamoja na kifo cha mmoja wa wanandoa,  talaka ambayo tunaiongelea  lakini  pia yapo mazingira  mengine mengi. 

        2.   AINA   ZA   TALAKA

Talaka twaweza kuzigawa katika makundi mawili nayo ni, talaka itolewayo nje ya mahakama ambayo hutokana na ndoa zilizo katika mfumo wa kimila na nyingine ni talaka itolewayo  mahakamani ambayo sisi hapa tutaiongelea. 

        3.   UKITAKA    TALAKA    FUATA    HATUA   HIZI.

( a ) Hatua ya  kwanza kabisa kwa anayehitaji kupata talaka ni  kupeleka malalamiko yako kwenye kitengo maalum kijulikanacho kama Bodi ya usuluhishi wa ndoa ambayo imeanzishwa na Sheria ya ndoa kifungu cha 102(1). 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...