Na Bashir Yakub
Yapo mambo  ambayo huwaumiza  watu vIchwa  yumkini  yakiwa   ni mambo madogo na ya kawaida.  Tatizo mara nyingi  huwa ni taarifa. Taarifa  zikimfikia  mtu ndipo huhisi jambo  ambalo alikuwa halijui  kuwa ni jepesi. 

Lakini kabla  ya taarifa mtu  huendelea kufikiria jambo hilo kwa ugumu. Katika kipindi kama hiki kuwa na kitu kama pasipoti si jambo la  anasa  au ufahari tena isipokuwa ni jambo  ambalo limeishaingia katika matumizi ya kawaida   ya kila siku ya walio wengi. 
Hii ni kutokana na kukua kwa  biashara za kimataifa, mawasiliano, utalii,usafirishaji  na kila kitu ambacho husababisha  watu kutoka nchi moja hadi nyingine.  Kwasasa kuwa na pasipoti  hata kama huna safari ya hivi karibuni ni jambo muhimu sana. 
Yumkini  usisubiri ikutokee safari ya ghafla halafu ndio uanze kukimbizana  na  pasipoti. Pasipoti inayo manufaa mengi  lakini moja ni kuwa pasipoti  ni mali kama mali nyingine. Pasipoti inaweza kumdhamini mtu kama  mali nyingine inavyoweza kumdhamini  mtu.Pasipoti  ni amana tena amana ya kuaminika. Ni  kutokana na umhimu huu nikaona leo nieleze  pasipoti na namna ya kupata pasipoti. Kusoma Zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...