NA  BASHIR  YAKUB-

Upo wakati kwenye  ndoa ambapo mmoja  wanandoa  anaweza akawa anataka  kuuza au kubadili jina la nyumba/kiwanja  bila ridhaa ya mwenzake ilihali  nyumba  hiyo  ni ya  familia. Lakini  pia  nje ya  hilo kuna  mazingira  ambayo  mtu anaweza  kuwa  si  mwanandoa lakini ana maslahi  katika  nyumba au  kiwanja cha mtu fulani  na anataka  kuzuia  nyumba/ kiwanja  hicho  kisibadilishwe  jina au kisiuzwe.  Kisheria jambo hilo linaruhusiwa  na huitwa zuio( Caveat).

Hili sio zuio la kwenda mahakamani  kama  mazuio tuliyoyazoea.Hili  ni zuio jingine  kama  nitakavyolieleza. Aidha  kuzuia hati  isibadilishwe  kimsingi ni sawa na  kuzuia nyumba isiuzwe.  Hii ni kwakuwa  hakuna namna ambavyo  mnunuzi anaweza kununua  kitu ambacho  hakiwezi  kubadilika  na kuingia  katika  jina  lake. Ikiwa  mke ana wasiwasi kuwa mume  anaweza kumzunguka  na kuuza mali ya familia  au mume ana wasi wasi juu ya uwezekano  wa mke kuuza basi wanayo  ruhusa  ya kuweka zuio ili hati  ya  nyumba  isibadilishwe.  Yapo mambo mengi kuhusu hili nitaeleza baadhi.
      
  1.         NINI  MAANA  YA  ZUIO.

Zuio ni usitishwaji wa muda ambao huwekwa ili kuzuia mabadiliko yoyote katika hati. Kama maana  yenyewe inavyojieleza  huu unakuwa ni usitishwaji wa muda  ambao unalenga  kulinda  maslahi ya  mtu aliyeomba  zuio.Kuitwa  zuio  la  muda haimaanishi  kuwa  mtu akizuia   itakuwa  ni mwezi mmoja  au  miwili basi, hapana. Ni  zuio  la  muda  kwakuwa  haliwezi kukaa milele  lakini  mtu akishaliweka  linaweza  kukaa  hata  miaka  mingi  kutegemea  na  sababu  za  zuio  hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...