Na  Bashir  Yakub.

Watu wengi wamenunua viwanja/nyumba  lakini mali hizo zimeendelea  kubaki katika  majina  ya waliowauzia. Wapo ambao  imepita  hata  miaka  kumi  tangu wanunue  maeneo   lakini  bado  hawajabadili  jina kuingia  jina  lake. Zipo sababu  nyingi  zinazosababisha  hali hiyo  lakini  moja  ni  watu  kutokujua  umuhimu  wa kubadili  jina  kwa haraka. 

Hapa sizungumzii  tu  kubadili jina  isipokuwa nazungumzia  kubadili  jina  kwa haraka. Kupitia  makala  haya  napenda  kuwaamsha  watu kuhusu  umuhimu mkubwa wa  kubadili  jina  kwa haraka  iwapo umenunua nyumba/kiwanja  kwa  mtu. Ni muhimu  sana  kufanya  hivyo  na itakuepusha na mambo mengi. 

1.KAMA  HUJABADILI   JINA  ALIYEKUUZIA   BADO   NDIYE   MMILIKI.

Ikiwa  kutatokea  mgogoro  wa umiliki  wakati ambao umenunua  nyumba/kiwanja  na  hujabadili  jina  kwenda  kwenye  jina  lako   kuna  hatari  kubwa zaidi  ya  kupoteza  ulichonunua. Hii ni kutokana  na ukweli kuwa utapokuwa  unatatuliwa  mgogoro  wa nani mmiliki  swali la  kwanza  huwa ni nani   ambaye  nyaraka  ya umiliki ina  jina lake. 

Yule  ambaye  jina lake  linaonekana  kwenye  hati au  leseni  ya  makazi  ndiye  hupewa  kipaumbele   na kwa mujibu  wa sheria  mwenye  jina  kwenye  hati  au leseni  ya  makazi  ndiye mmiliki. Wewe  uliyenunua  utakuwa  na mkataba  na  jina  lako litakuwa  kwenye  mkataba lakini  pamoja  na kuwa  na jina kwenye mkataba  bado  huwezi  kulinganisha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...