Mkuu wa wilaya Temeke, Sofia Mjema, akizungumza na wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Kiislamu, Twayyibat, iliyopo Manispaa ya Temeke, jijini Dar es Salaam, wiki iliyopita.
Kuwapo kwa
shule hizo kutazidi kuongeza idadi kubwa ya watoto wanaopata elimu ya msingi,
sekondari na vyuo Vikuu kwa ajili ya kujikomboa katika maisha yao.
Ukiacha
mikoani ambako hakuna shule nyingi hususan maeneo ya vijijini, jijini Dar es
Salaam kumefanikiwa kuwa na shule nyingi mno, zikiwamo za serikali na
mashirika.
Zipo shule
za kidini ambazo wakati wote zimekuwa zikifundisha watoto elimu ya Dunia na ile
ya kufahamu Mungu ni nani, nazumgumzia pale watoto wanapofundishwa kisawa sawa
na kukolea kiimani kama njia ya kumjua Mungu na kutenda matendo ya kiungwana.
Mwishoni mwa
wiki iliyopita, Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sofia Mjema, alitembelea katika shule
ya Twayyibat Islamic Seminary, iliyopo Temeke, jijini Dar es Salaam.
DC Sofia
alitumia muda huo kuikagua shule hiyo pamoja na kuzungumza na wadau wa elimu,
walimu na wanafunzi wa shule hiyo kwa ajili ya kuona inakuwa kati ya shule bora
wilayani Temeke na Dar es Salaam kwa ujumla.
Miongoni mwa
mambo yaliyomkosha DC Sofia ni pale alipoambiwa kuwa ada ya shule hiyo kwa
mwaka mmoja ni Sh 200,000 tu, jambo ambalo ni agharabu kuliona wala kulikisia
katika shule mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
shuleni hapo, Mkuu huyo wa wilaya ya Temeke, Sofia, anasema kwamba ameshangazwa
na kuwapo kwa ada nafuu katika shule ya Twayyibat.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...