Kwa heshima na taadhima mnakaribishwa kwenye hadhara ya kuadhimisha mazazi ya Mtume Muhammad Allah amuiye radhi.

Hadhara itafanyika siku ya Jumamosi sawa na tarehe 21/02/2015  kwenye anuani ifuatayo ‘4O GOLDSMITH ROAD NN8 3RU’ kuanzia saa nane mchana hadi saa moja usiku.

Masheikh kutoka sehemu mbalimbali wamealikwa kwa malengo ya kuilezea historia ya Mtume Muhammad (SAW) kwa kina. Sheikh Muhammadul Eid (Abu Eid) ataongoza shughuli hiyo kama mgeni rasmi.  Pamoja na mambo mengine hadhara ina malengo ya kuikutanisha jamii, kuwakumbusha watu wazima na kuwafundisha watoto tabia za Mtume (SAW) kama vile uaminifu ukweli na nyinginezo ili waweze kujifananisha nae. 

Itakumbukwa kwamba sheikh Abu Eid yuko nchini Uingereza karibu wiki mbili sasa ktk ziara ya kida’wa na amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuzidisha mshikamano khususan ktk jamii zinazozungumza Kiswahili.

Kwa wakazi wa Uingereza na hasa maeneo ya jirani mnahimizwa kujitokeza kwa wingi ili muweze kufadika na nasaha kutoka kwa masheikh mbalimbali. Kwa mawasiliano kuhusu shughuli unaweza kupiga na zifuatazo 07529302674 au 07986142485. 

Wote mnakaribishwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...