MWIMBAJI wa kimataifa raia wa Uingereza, Ayobami David  ni mmoja wa waimbaji wanaopenekezwa sana na mashabiki waalikwe katika onesho la miaka 15 ya Tamasha la Pasaka nchini.
 
Ayobami ni mwimbaji ambaye anafanya vizuri katika muziki huo wa Kumtukuza Mungu kupitia nyimbo  mbalimbali.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama alisema katika taarifa yake kuwa mwaka huu wanataka kutoka kivingine.
 
“Mashabiki wamekuwa wakiomba tumualike Ayobami, bado tunapokea maoni mbalimbali na kulingana na vigezo vyetu tutajipanga,” alisema Msama. Alisema kwa kuwa wameamua kukuza muziki huo hapa nchini, wataalika wasanii mbalimbali wa kimataifa ili kulifanya tamasha la mwaka huu liwe la aina yake.
 
Alisema wamekuwa wakiwatumia katika matamasha yake yaliyoasisiwa tangu mwaka 2000, waimbaji kutoka Kenya, Zambia, Afrika Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na wa hapa nchini.
 
“Niliyoeleza mwanzoni yanakamilika, kwa sababu nilidhamiria kuliboresha zaidi Tamasha la Pasaka kwa kuwashirikisha waimbaji wa Kimataifa, mashabiki wakae mkao wa kula kupata ladha tofauti katika tamasha la mwaka huu,” alisema Msama.  
 

Baadhi ya waimbaji waliopata kutumbuiza Tamasha la Pasaka tangu lianzishwe ni Rebecca Malope, Keke Phoofolo (Afrika Kusini), Ephraim Sekereti (Zambia), Faraja Ntaboba (DRC) na Sarah K, Paul Mwai (Kenya).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...