Mgeni rasmi kwenye mafunzo ya stadi za kazi na utambuzi wa fursa za kiuchumi zilizopo mkoa wa Lindi Naibu waziri wa kazi na ajira mhe.Dr. Makongo Mahanga (MB) amewataka vijana wa mkoa wa Lindi kuyageuza mafunzo watakayoyapata ya stadi za maisha sanjari na kuzitambua fursa zilizopo ndani ya mkoa, waweze kujiajiri na kujikomboa kiuchumi,wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo ambapo jumla ya vijana 360 kutoka halmashauri sita zilizopo mkoani Lindi wameudhuria kwenye ukumbi wa kanisa katoliki Mt.Kagwa. Vijana 360 kutoka kwenye wilaya za Kilwa,Ruangwa,Liwale,Nachingwea,Lindi Mjini na Vijijini ambao ni washiriki wa mafunzo wakimsikiliza kwa makini mgeni rasmi naibu waziri wa kazi na ajira Mhe.Dr.Mkaongoro Mahanga hayupo pichani.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe.Mwantumu Mahiza akiwaeleza washiriki wa mafunzo ya stadi za maisha sambamba na kufahamu fursa za kiuchumu ambapo mpango wa kuendesha mafunzo hayo umebuniwa na yeye mwenyewe,mbele ya mgeni rasmi,wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...