WATUMISHI wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, (NHIF) wametakiwa kushikamana kwa pamoja na kufanya kazi bila kujali muda wa kazi ili kuhakikisha shirika hilo linabaki na heshima yake huku wanachama wakihudumiwa kwa heshima.

Rai hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Bw. Emanuel Humba katika hafla ya kuaagwa wastaafu wa Mfuko huo.

Bw. Humba ambaye naye alikuwa ni miongoni mwa waagwa, alisema kuwa mbinu kubwa ya kushinda katika utenda kazi kushikamana na kufanya kazi kwa ushirikiano bila kujali hali ya aina yoyote.

“Nawaombeni wafanyeni kazi kwa ushirikiano, Menejimenti wajalini watumishi na ninyi kwa ninyi kuweni kitu kimoja, sisi tumeacha heshima kwa shirika kwa kuwa tulifanya kazi bila ubaguzi na tulishirikiana sana,”

 “Nitahudhunika sana nikiona au kusikia shirika hili likifa au kudorola, sisi wenzenu nikiwemo mimi ambaye ni mwanzilishi sitakubali kuona hali hii kwa kuwa nimewekeza nguvu kubwa sana ndani ya Mfuko huu, watumikieni Watanzania kwa heshima ili lengo la kuanzishwa kwa Mfuko huu lisipungue,” alisema Bw. Humba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...