Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Semamba Makinda (Mb), kwa niaba ya Bunge la Jamhuri ya Muungao wa Tanzania anatuma salaamu za rambirambi kwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Bwana Othman Rashid, kufuatia kifo cha mama yake mzazi, BI. TAJIRI ABDALLAH KITENGE, kilichotokea tarehe 5 Februari, 2015.

Aidha, Spika Makinda anatuma salaamu za rambirambi kwa Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania Mhe. Augustino Ramadhani kufuatia kifo cha mama yake mzazi, BI. BRIDGET RAMADHAN, kilichotokea Februari 3, 2015.

“Nimepokea taarifa za misiba hii kwa masikitiko makubwa na ninawapa pole familia, ndugu, jamaa na marafiki wote. Ninamwomba Mwenyezi Mungu awape faraja wafiwa katika kipindi hiki kigumu.

BWANA  alitoa na BWANA  ametwaa, Jina la BWANA  lihimidiwe. Amina.”


Imetolewa na Ofisi ya Bunge,
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na
Uhusiano wa Kimataifa

DODOMA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...