Baadhi ya Askari wa Jeshi la Polisi Tanzania wakitoa heshima mbele ya jeneza lililobeba Mwili wa Marehemu Mzee Andrew Michael Kumalilwa ambae alikuwa mstaafu wa jeshi la Polisi kwa ngazi ya DCP
Ndugu wa marehemu akijadiliana jambo na Mmoja wa Askari wa Jeshi la Polisi wakati wa Kutoa Heshima za mwisho kabla ya kwenda kuupumzisha mwili wa Mzee Andrew Kumalilwa ambae alizikwa nyumbani kwake Tabata Segerea tarehe 14 Februari 2015.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani na Jeshi la Polisi Tanzania, DCP Simon Siro akitoa maneno mafupi kabla ya kwenda kuupumzisha Mwili wa marehemu Mzee Andrew Kumalilwa katika nyumba yake ya Milele. Marehemu Andrew Kumalilwa alizikwa mnamo tarehe 14 February 2015 huko Nyumbani Kwake Tabata Segerea.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...