WAZIRI wa Uchukuzi, Samuel Sitta ameelezea kufurahishwa na waandaaji wa Tamasha la Pasaka na kusema kuwa katika miaka 15 ya tamasha hilo wana mengi ya kujivunia.
 
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa Dar es Salaam jana na kusainiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama ilieleza kuwa kamati yake imepokea salamu kutoka kwa Waziri Sitta akizungumzia maandalizi ya miaka 15 ya tamasha hilo.
 
“Ni tamasha lenye tija kwa Watanzania, mimi mwenyewe nimekuwa shahidi wa namna mnavyosaidia yatima, wajane na makundi mbalimbali ya kijamii.
 
“Nimesikia mwaka huu mna tamasha kubwa la miaka 15 tangu muanze kufanya Tamasha la Pasaka, niwatakie kila la heri katika maandalizi na naamini litakuwa tamasha la aina yake,” alisema Msama katika taarifa yake akimnukuu Sitta.

Alisema wamekuwa wakipokea salamu kutoka kwa wadau mbalimbali wakizungumzia kuhusiana na maandalizi ya Miaka 15 ya Tamasha la Pasaka na wakielezea pia mafanikio mbalimbali yaliyopatikana kwa kipindi hicho.

Baadhi ya walioguswa na maandalizi ya tamasha hilo ni waimbaji mahiri wa muziki wa Injili kutoka Afrika Kusini Solly Mahlangu ‘Obrigado’ na Rebecca Malope.

 Wasanii hao wamewahi kwa nyakati tofauti kuja nchini katika Tamasha la Pasaka, ambapo mwaka huu waandaji wamepanga kufanya sherehe ya Miaka 15 ya Tamasha la Pasaka.

   

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...