Na Woinde Shizza,Arusha
Sekta ya madini nchini bado inakabiliwa na changamoto mbalimbali
ikiwemo uhaba wa walimu na wataalamu wa kufundisha namna ya ukataji wa vito vya
madini hali inayosababisha kuuzwa kwa madini ghafi nje ya nchi na
kupelekea kuuzwa kwa bei ya chini na pesa nyingi kwenda nje ya nchi .
Hayo yameelezwa na mratibu wa kituo cha Jimolojia Tanzania,Musa
Shanyangi wakati akiongea na waandishi wa habari katika kituo hicho kinachotoa mafunzo ya ukataji madini ya vito,ambapo wameanza kutoa mafunzo
ngazi ya cheti kwa wahitimu 15 wakike ambapo chuo kipo katika
halmashauri ya manispaa ya jiji la arusha.
Alieleza kuwa hivi sasa madini ghafi yanauzwa sana nje ya nchi kwa bei
ya chini lakini kama wangeweza kuuza madini hayo yakiwa yameongezwa
thaman na kuuzwa kwa bei ghali na kuwezesha fedha za kigeni kubaki
nchini na kuongeza pato la taifa .
Shanyangi aliongeza kuwa hivi sasa wameanza kuwafundisha kozi ya miezi
6 kwa wanafunzi 15 wakike ambapo wanafadhiliwa na Arusha Women Foundation Fund iliyoko mjini ikiwa na lengo la kuwasaidia mabinti ili
kuweza kusaidia sekta ya madini na kuweza kukabiliana na uhaba wa
wataalamu wa ukataji madini nchini.
Hata hivyo kituo hicho kinatarajia kuongeza wanafunzi mpaka kufikia 60
ili kuweza kuongeza ufanisi na kuweza kuboresha sekta hiyo ya madini
ili kuweza kuongeza wataalamu ,pia wanamkakati wa kuweza kusomesha
walimu wazawa ili kuweza kukidhi nakuwa na walimu na kupunguza gharama
za kuchukua mwalimu kutoka nje yanchi ambapo hivi sasa wamemuajiri
raia kutoka Sri lanka hali ambayo wanatumia gharama kubwa kumlipa
mtaalamu huyo toka nje ya nchi.
Shanyangi aliwataka wadau mbalimbali nchini pamoja na wawekezaji
wawekeze katika kufundisha wataalamu wazawa ili kuweza kukidhi
mahitaji ya wakataji na wataalamu nchini.
Kituo hicho kimegharimu zaidi ya shilingi billion 1.2 na mashine
mbalimbali za kituoni hapo zimegharimu zaidi ya milioni 450 za ukataji
na kusafisha madini hayo.
Kwa upande wake mwanafunzi katika chuo hicho
Bi.Joice Patrick alisema kuwa kupitia mafunzo hayo ya ukataji wa
madini na ung'arishaji itawasaidia katika swala zima la ajira huku
akiwataka wanawake kuchangamkia fursa hiyo "Ni fursa sasa kwa wanawake
kujitokeza katika kazi hii na waione kama kazi zingine na si kuwaachia
wanaume tu "alisema Joice.
Mmoja wa wanafunzi katika kituo cha Jimolojia Tanzania,Grace Charles akiendelea na ukataji wa madini huku akitumia kifaa maalumu.
Wanafunzi Gladness John pamoja na Loveness Marteen wakiwa wanaendelea na shughuli ya ukataji.
Magret Joseph akiwa anaangalia kwa makini namna alivyokuwa akikata jiwe kwa kutumia mashine maalum.(picha zote na Woinde Shizza,Arusha)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...