Ulikuwa ni usiku wa manane majira ya saa nane na nusu, ambapo Mzee Jengo alikuwa amepumzika kitandani akiwa na mtoto wake wa kiume ambaye alikuwa anaitwa Rony.
Alikuwa ni kijana mdogo mwenye umri  kati ya miaka nane au tisa, Usiku huo hali ya Mzee Jengo ilikuwa si nzuri kwani alianza kujisikia vibaya ghafla kiasi kwamba hata alipojaribu kunyanyuka alishindwa. Kutokana na maumivu makali aliyokuwa akiyasikia aliamua kumuamsha mtoto wake, taratibu alinyoosha mkono na kuanza kumvuta Ronyhuku akizungumza kwa sauti ya unyonge sana.



 “Rony, Rony …..aaaaa…amka ukamwambie ….dada mimi naumwa, Rony mwanangu nenda kamwite dada yako najisikia vibaya sana” Alikuwa akizungumza kwa shida sana, lakini Rony alimsikia, na kwa haraka aliamka huku akiwa anafikicha macho yake kutokana na kushtuka kutoka usingizini, alimtizama baba yake, na moja kwa moja alishuka kutoka kitandani huku akiwa anamuuliza Baba yake, “Baba unaumwa nini,  nani atakupeleka hospitali Baba,”. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...