Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mhe. Dani Makanga akizungumza na wajumbe kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo waliofika ofsini kwake kwa ajili ya kujitambulisha kabla ya kuendelea na ratiba yao ya mafunzo kwa Vijana wa Halmashauri za Kasulu na Bihigwe leo mjini Kasulu. Katikati ni Mkuu wa msafara huo ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Esther Riwa na wa kwanza kushoto ni Afisa Vijana wa wizara hiyo Bi. Amina Sanga.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Bw. Bernard Ntikabuze (kushoto) akiagana na akipeana mkono na Afisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga wakati walipotembelea ofisini kwa Mkurugenzi huyo leo. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Esther Riwa.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kasulu Bw. Muguha Titus Muguha akizungumza na Vijana wanaoshiriki mafunzo kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (hawapo pichani) yanayotolewa na wataalamu kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. Kutoka kulia ni Afisa Vijana wa Wizara hiyo Bi. Amina Sanga, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria Bibi. Esther Riwa, Mkuu wa Kituo cha Maendeleo ya Vijana Sasanda kilichopo Mbeya Bw. Laurian Massele na Afisa Vijana wa Mkoa wa Kigoma Bw. Edward Manase.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...