Wananchi wa mji wa Ilula katika wilaya ya Kilolo mkoani Iringa leo wamezua tafrani dhidi ya Askari Polisi baada ya mwanamke mmoja kupoteza maisha kwa kudaiwa kusababishwa na Askari hao waliokuwa kwenye msako wa kukamata watu wanaokunywa pombe wakati wa kazi.

Kutokana na tukio hilo, mwanamke huyo aliyepoteza Maisha aliyetambulika kwa jina la Mwanne Mtandi awali aliamua kukimbia kwa lengo la kukwepa kukamatwa na Polisi hao Kabla ya kukutwa nyuma ya jengo la kilabu hicho cha pombe za kienyeji kilichopo mtaa wa Ilala Mjini Ilula akiwa amekufa.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa,Tukio hilo lilitokea majira ya saa 5 asubuhi leo na kudumu hadi Majira ya saa 10 jioni huku kituo cha Polisi kilichopo kwenye mji huo kudaiwa kuvunjwa na kuchomwa moto kwa magari matatu na Pikipiki Moja ya polisi.
Baadhi ya wananchi wa mji wa Ilula katika wilaya ya Kilolo mkoani Iringa wakiwa wameizunguka moja ya gari linalodaiwa kuchomwa moto na baadhi yao kufuatia vurugu kubwa iliyotokea mapema leo.
Moto ukiendelea kuwaka barabarani.
Vurugu hizo zilisababisha wasafiri wanaotumia barabara ya Kuu ya Mikoa ya Nyanda za juu kusini kukwama kwa zaidi ya masaa 6.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...