Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba (kushoto) akimsimika kwa kumkabidhi fimbo ya ulezi baada ya kumvalisha joho, kofia na skafu, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, mkoani Lindi, Mathias Chikawe, kuwa mlezi wa UWT katika wilaya yake ya Nachingwea. Sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wanachama wa UWT, ilifanyika katika Ukumbi wa NR mjini Nachingwea leo. Wapili kulia ni Mkuu wa wilaya hiyo, Regina Chonjo, na wapili kushoto ni mwanachama wa UWT wilayani humo, ambaye pia ni Mke wa Waziri Chikawe, Profesa Amandina Lyamba
 Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo (kushoto), Mke wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe, Profesa Amandina Lyamba (kulia) wakilisakata rumba na wanachama wenzao wa Umoja wa Wanawake (UWT) wilayani humo baada ya Mbunge wao kusimikwa rasmi na Mwenyekiti wa UWT Taifa, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, kuwa mlezi wa UWT katika wilaya yake ya Nachingwea. Sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wanachama wa UWT, ilifanyika katika Ukumbi wa NR mjini Nachingwea leo.
 
 Mlezi wa Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Nachingwea, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kushoto), akipokea zawadi kutoka kwa mwakilishi wa UWT wilayani humo baada ya Waziri huyo kusimikwa na rasmi na Mwenyekiti UWT Taifa, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba (kushoto kwa Chikawe), kuwa mlezi wa UWT wilayani humo. Sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wanachama wa UWT, ilifanyika katika Ukumbi wa NR mjini Nachingwea leo
 Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba akizungumza kwa furaha wakati akitoa hotuba yake kwa wananchama wa UWT Wilaya ya Nachingwea baada ya kumsimika Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kushoto) kuwa mlezi wa UWT wilayani humo. Sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wanachama wa UWT, ilifanyika katika Ukumbi wa NR mjini Nachingwea leo. Katika hotuba yake hiyo, Waziri Simba alimuomba Waziri Chikawe aendelee kuisaidia UWT wilayani humo kama alivyokuwa anafanya awali. Kulia ni Mwenyekiti wa UWT, Mkoa wa Lindi, Faudhia Chiwangu.
 
 Mlezi wa Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Nachingwea, ambaye pia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akiwashukuru wanachama wa UWT wilayani humo kwa kumchagua kuwa mlezi wa umoja wao katika sherehe ya kusimikwa kwake iliyofanyika mjini Nachingwea leo. Katika hotuba yake, Waziri Chikawe ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, aliwaomba wanachama hao kuwa na ushirikiano kwa kuijenga CCM, pamoja na kuhakikisha wanawahamasisha wananchi jimboni humo kujiandikisha katika daftari la wapiga kura ili kujiandaa kwa kuipigia kura Katiba iliyopendekezwa pamoja na Uchaguzi Mkuu ujao. Kulia ni Mwenyekiti UWT Taifa, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba ambaye alimsimika mlezi huyo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Regina Chonjo

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba (kushoto) akimsimika kwa kumvalisha joho la ulezi Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, mkoani Lindi, Mathias Chikawe, kuwa mlezi wa UWT katika wilaya yake ya Nachingwea. Sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wanachama wa UWT, ilifanyika katika Ukumbi wa NR mjini Nachingwea leo. Picha zote na Felix Mwagara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...