Naibu waziri wa maji Amos Makalla amefanya ziara ya kikazi wilayani Hanang leo kwa kutembelea mradi wa maji kijiji cha Ishponga na kuagiza Generator lifungwe haraka kurejesha huduma ya maji iliyosimama kwa miezi mitatu 
Amekagua mradi maji Kateshi na kuhaidi kushughulikia tatizo la nishati ya umeme linalopelekea mamlaka kushindwa kumudu gharama za uendeshaji 
Ameweka jiwe la msingi mradi mkubwa wa maji kijiji cha Simbay kata na tarafa ya Simbay Aidha ameagiza mradi wa mradi wa maji wa Endasak utakaohudumia vijiji vitatu wiki ijayo halmashauri itangaze zabuni za kumpata mkandarasi kwani tayari wizara imeshatuma shilingi milioni 300 Ameagiza watu 39 waliovamia chanzo cha maji Endasak wapewe notisi waondoke eneo la chanzo
Naibu waziri wa maji Mhe. Amos Makalla akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Frederick Sumaye huko Hanang leo
Naibu waziri maji Amos makalla akiweka jiwe la msingi mradi maji kijiji cha Simbay- Hanang
Naibu waziri maji kushoto na mbunge wa Hanang wakiwasikiliza viongozi wa kijiji cha Ishponga

Naibu waziri Amos Makalla akizungumza  na mbunge wa Hanang na waziri ofisi ya Rais (Mahusiano)  Dr Mary Nagu
Naibu waziri maji akikagua tanki la maji mji wa Katesh

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...