WADAU 100 waliofanikisha kwa namna mbalimbali  katika kipindi cha miaka 15 tangu kuanzishwa Tamasha la Pasaka nchini wanatarajiwa kupewa tuzo wakati wa tamasha la mwaka huu.
 
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama ilieleza kuwa wadau hao ni wanasiasa, viongozi wa dini, wafanyabiashara na waandishi wa habari.
 
“Wapo wengi waliotusaidia kufikia hapa tulipo, lakini tumeteua 100 hawa watapokea kwa niaba ya wengine, ikiwa ni shukrani kwa kutusaidia kwa namna mbalimbali.
 
“Wapo waliotusaidia wanatoka Dar es Salaam na wengine mikoani, hivyo wale wa mikoani tutawapa tuzo zao wakati tukienda katika matamasha ya huko na wale wa Dar es Salaam watapokea siku yenyewe ya Pasaka,” alisema Msama.
 
Alieleza kuwa si kazi rahisi kuweza kusimamisha tamasha kubwa kama hilo kwa miaka 15, pia si kazi ya yeye peke yake bali ni ushirikiano wa watu mbalimbali ambao anaona kuna umuhimu wa kuwashukuru.
 
Alisema watawapa tuzo maalum pamoja na vyeti ambavyo anaamini kwa kiasi fulani vinaweza kuwafanya wahisi kweli mchango wao umetambuliwa.
 
Mwaka huu Tamasha la Pasaka linatimiza miaka 15 tangu lianzishwe, ambapo waandaaji wamepanga tamasha kubwa la kuendena na sherehe hizo.
 

Tayari wasanii maarufu kutoka nje ya Tanzania wameshathibitisha kushiriki  wakiwemo Rebecca Malope na  Solly Mahlangu ‘Obrigado’ wote kutoka AAfrika Kusini na raia wa Uingereza Ifeanyi Kelechi 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...