UONGOZI wa Simba umemtangaza mwandishi wa habari wa siku nyingi,Haji Sunday Manara kuwa msemaji mpya wa klabu hiyo ya wekundu wa Msimbazi.
Katibu mkuu wa Simba Steven Ally ameiambia Globu ya Jamii kuwa Manara atachua nafasi ya Humphrey Nyasio ambaye atapangiwa majukumu mengine.
"Kamati ya Utendaji ya Simba imemkabidhi jukumu Manara baada ya kujiridhisha pasi na shaka uzoefu wake katika masuala ya michezo na pia uzoefu wake katika mambo mbalimbali ya kiutawala, hivyo kuwa na imani kwamba ataifanya kazi yake vizuri kama walivyofanya watangulizi wake."alisema Ally.
Hongera Haji!!! Sasa piga kazi usifanye yale mambo ulipokuwa diwani. Mdogo wako Sakina yupo wapi siku hizi?
ReplyDeleteMchizi wangu wa Bunge huyu 7A poa sana kaka piga kazi!!
ReplyDelete