Licha ya kusemwa sana kwa muda mrefu juu ya kuhusishwa na chama kipya cha siasa cha ACT-Tanzania dhidi ya aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Ruyagwa Kabwe (pichani juu akisaini kitabu baada ya kupewa kadi) sasa yamekuwa kweli kwa Mbunge huyo baada ya jana  Jumamosi ya Machi 21, kupokelewa rasmi na chama hicho na kukabidhiwa kadi yake yenye namba 007194.

Hili limetokea  siku moja tu baada ya Zitto kutangaza kuachia ubunge na kuandika barua rasmi ambapo sasa amekuwa mwanachama wa ACT-Tanzania na kuahidi kuendeleza mapambano ndani ya chama hicho.


 ACT-Tanzania: kirefu chake ni Chama cha Alliance for Change and Transparence Makao makuu ya chama hicho yapo Kijitonyama Jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. nahitaji card haraka sana nitaipataje ikiwa niko ughaibuni???

    ReplyDelete
  2. Hapo Zitto kadhihirisha kuwa wapinzani kamwe hawashinda kura ya urais tanzania 2015 na daima. Maana wananchi wa kigoma aliwawakilisha kama mbunge watahama chadema na kuhamia ACT- Tanzania. ACT siyo chama chenye nguvu kwa sasa Tanzania, ni zitto tu anataka ubunge tena 2015. Sasa Watanzania lazima mkubali uroho wa madaraka sio CCM tu hata wapinzani.

    ReplyDelete
  3. Zitto alifukuzwa uanachama Chadema.

    ReplyDelete
  4. Zitto hakufukuzwa. Katiba ya chadema inasema "mwanachama akiipeleka chadema mahakamani akashindwa, atakuwa amejivua uanachama wake" kwa hiyo alivyoshindwa mahakamani automatically anakuwa sio mwanachama tena.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...