Na Bashir
Yakub.
Watu wengi wanaonunua
ardhi wamekuwa wakipata
usumbufu mkubwa katika kubadili
majina yaani kutoka mmiliki
wa mwanzo kwenda
kwa mmilki mpya aliyenunua. Upo usumbufu ambao husababishwa
kwa makusudi na maafisa
wanaohusika lakini pia
upo usumbufu ambao husababishwa na watu wenyewe
wanaotaka kubadili majina.
Awali ya yote
lazima nikiri kuwa
baadhi ya maafisa
wa mamlaka za
ardhi husababisha uchelewaji
kwa makusudi kabisa
na lengo likiwa kujenga mazingira
ya kupozwa kidogo.
Hili lipo
na kila mtu
ambaye amekuwa akishughulikia masuala
ya hati na
kubadili majina miliki
kama mimi atakiri
kukutana na haya. Hao tuwaache
mimi leo nazungumzia
maandalizi ambayo ukiyafanya
mapema utafanikiwa kwa
urahisi na haraka kubadili
jina la
kiwanja au nyumba
kutoka kwa mtu akiyekuuzia kuingia jina
lako.
1.UMUHIMU WA
KUBADILI JINA HARAKA BAADA
YA MANUNUZI.
Sheria iko wazi kuwa
ambaye jina lake
linaonekana kwenye hati
ndiye mmiliki.
Kwa kauli hii mnunuzi
anatakiwa kufanya
jitihada za haraka
na za makusudi kubadili
jina mara tu baada ya
kununua kiwanja au
nyumba. Sikatai kuwa kunakuwa
na mkataba wa mauziano
lakini lazima ieleweke
kuwa mbele ya macho ya
sheria jina lililo
kwenye hati lina
uzito kuliko mkataba
wa mauziano.
Usiridhike kukaa
na mkataba wa
mauziano ikiwa hujabadili
jina. Hii ni kwa
ajili ya ulinzi
wako na wa
ardhi yako. Utakapotokea mgogoro
wa umiliki ikiwa
hujabadili jina waweza kuwa
katika hatari kubwa
ya kupoteza hasa
kama mgogoro huo umeanzishwa
na aliyekuuzia. Huu ndio ukweli na
lazima tuonyane ili
tuwe salama na mali
zetu.
Lakini pia hata ukitokea
mgogoro mwingine wowote
wa umiliki kuna
mambo ndani ya
sheria yataufanya kuwa mgumu kutokana na sababu
tu kuwa ulikuwa hujabadili jina.
Hapo sijaongelea faida
nyingine za kubadili jina
kama kukopa n.k. Nishauri
tu kwa ufupi
kuwa unapojiandaa kununua
nyumba au kiwanja jiandae
pia na kubadili jina
moja kwa moja.
Hakikisha haya mawili
yanakwenda pamoja. Kusoma zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...