Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikatisha kwenye migomba alipokuwa akikagua mifereji ya inayotiririsha maji kuelekea kwenye mashamba ya ndizi akiongozana na Mh. Agrey Mwanri.
Akielezea utekelezaji wa ilani ya uchaguzi katika jimbo hilo Mh. Agrey Mwanri amesema ilani ya CCM imetekelezwa kwa kiwango kikubwa ambapo vijiji vyote katika jimbo hilo vina maji safi na salama ya kunywa, Umeme umefika katika vijiji vyote kinachondelelea ni usambazaji kwa kila mwananchi, Suala la huduma za afya nalo liko vizuri kwani vimejenga vituo vya afya karibu kila maeneo na baadhi ya zahanati zinamaliziwa kujengwa.
Suala la Elimu wakati mbunge huyo akiinga madarakani Siha kulikuwa na sekondari moja, lakini sasa kuna sekondari 17 na ufaulu wa wanafunzi umeongezeka kwa kiwangi cha juu, Maabara zinakamilishwa ambapo mabati yamesambazwa karibu kila shule ili kukamilisha ujenzi wa maabara hizo.
Akizungumza katika mkutano huo pamoja na mambo mengine Katibu Mkuu wa CCM amemsifu Mh. Agrey Mwanri kwa kazi aliyoifanya katika jimbo hilo kwa kufanya kazi vizuri na kuwaletea wananchi maendeleo na kuwaambia wananchi katika mkutano huo kwamba kama kiongozi anafanya kazi nzuri hakuna haja ya kubadilisha viongozi kama mashati, Mwacheni awaleteeni maendeleo.Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoka kwenye chumba cha maabara cha hospitali ya wilaya Siha mara baada ya kuyakagua magari matatu ya kubebea wagonjwa.
Sehemu ya jengo la hospitali hiyo ya wilaya ya Siha kama lionekanavyo pichani,ambapo Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alikwenda kukagua.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo ya bwawa la umwagiliaji la Kishisha kata ya Ivaeny kutoka kwa mbunge wa jimbo hilo Mh. Agrey Mwanri wakati alipokagua bwawa hilo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akichukua ndizi wakati alipowatembelea akina mama wajasiriamali kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa CCM wa wilaya ya Siha.
PICHA NA MICHUZI JR-JIMBO LA SIHA KILIMANJARO.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
PICHA NA MICHUZI JR-JIMBO LA SIHA KILIMANJARO.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...