Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (katikati), akishiriki kuchimba shimo la choo cha Shule Mpya ya Msingi ya Kikwete, eneo la Chamwino Ikulu, Jimbo la Chilonwa wakati wa ziara yake ya siku tisa ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua miradi inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM, katika Wilaya ya Chamwino, Mkoa wa Dodoma leo.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akishiriki kupulizia dawa ya kuua wadudu katika mradi wa shamba la zabibu wa Chinangali II, wilayani Chamwino, mkoani Dodoma leo.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Mtera,Mh.Livingstone Lusinde ndani ya wilaya ya Chamwino mapema leo.
Sehemu ya jengo la Zahanati ya kijiji cha Mahampha katika kata ya Chilonwa,Wilayani Chamwino,ambapo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana alishiriki ujenzi wa zahanati hiyo
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiungana na vikundi vya ngoma kupiga ngoma alipowasili kwenye mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Majereko, wilayani Chamwino leo.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia katika mkutano huo wa hadhara.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana Katibu Mkuu wa CCM,akihutubia katika mkutano huo, ambapo alisema CCM ni chama pekee nchini kinachowajali wanawake kwa kuwapatia nafasi nyingi za uongozi. Leo ni maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani ambayo kitaifa imeadhimishwa mkoani Mororo na mgeni rasmi alikuwa Rais Jakaya Kikwete.

PICHA NA MICHUZI JR-CHAMWINO DODOMA.
Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...