Tume ya Taifa ya Uchaguzi inawatangazia wananchi wote wa Mkoa wa Njombe, kuwa itaanza zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa kutumia teknolojia ya “Biometric Voters Registration” kuanzia tarehe 16/03/2015 hadi tarehe 12/04/2015.   Aidha katika kata ya Utengule ya Mji mdogo wa Makambako Uboreshaji utafanyika kuanzia tarehe 9-15/03/2015. Uandikishaji huo utahusisha Halmashauri zifuatazo:-
Mkoa
Wilaya
Kata
Idadi ya Vituo
Tarehe Ya Uandikishaji
NJOMBE
NJOMBE TC
ZOTE

16/03 – 12/04/2015

WANGING’OMBE DC
ZOTE



NJOMBE DC
ZOTE



LUDEWA DC
ZOTE



MAKETE
ZOTE



MAKAMBAKO
UTENGULE
12
11-17/03/2015

Vituo vya Uandikishaji vitakuwa kwenye Vijiji, Vitongoji na Mitaa
 Watakaohusika katika zoezi hili ni wananchi wote:-
·         Waliotimiza umri wa Miaka 18 na  kuendelea  na wale wote  watakaotimiza miaka 18 ifikapo mwezi Oktoba, 2015.
·         Waliojiandikisha awali kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura la zamani ili kuhuisha taarifa zao na kupata kadi mpya za kupigia kura.
·         Wale wote ambao wanazo sifa za kujiandikisha  lakini hawajawahi kujiandikisha kwenye Daftari.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi inasisitiza wananchi wote wa Mkoa wa Njombe  kujitokeza kwa wingi kuanzia tarehe 16/03/2015 mpaka  tarehe 12/04/2015 kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ili kuwawezesha kupiga Kura ya Maoni na kuchagua Viongozi wao katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu 2015.
Vituo vya kujiandikisha vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 Asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni
Kumbuka:- Hutaweza kupiga Kura ya Maoni au Kupiga Kura wakati wa Uchaguzi Mkuu kama utakuwa hujajiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. 
Nenda kajiandikishe sasa. 

Tangazo hili limetolewa na
 Tume ya Taifa ya Uchaguzi, S.L.P. 10923, Dar es Salaam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...