Na Bashir Yakub.

Kuongezeka kwa makampuni na taasisi mbalimbali kumetengeneza wingi wa ajira maeneo mbambali ya nchi. Mbali na kuongezeka kwa ajira hizi kumekuwepo na tatizo kubwa la waajiriwa kutojua haki zao mbalimbali wawapo maeneo ya kazi.

Niseme jambo moja tu kuwa hakuna suala la msingi kama muajiriwa kujua haki zake. Hii ni kwasababu kupitia kujua haki zake ndipo anapoweza kupata ujira stahiki, posho stahiki, masurufu stahiki, mafao stahiki, malipo stahiki ya kuachishwa kazi ikiwa ni pamoja na ujumla wa kufanya kazi kwa misingi ya kazi.

Ni muhimu kila mfanyakazi kupitia pitia haki zake mara kwa mara ili kujua nini anapata na nini hapati. Uwe kazini au umeachishwa bado ipo nafasi ya kudai haki hizi ili upate kilicho chako.

Ukitegemea mwajiri ndio akwambie haki zako utakuwa unajidanganya kwasababu yawezekana kabisa faida kubwa ya mwajiri ipo katika wewe kutokujua haki zako. Ni hasara kubwa kufanya kazi bila kujua haki zako . Kutokana na hilo leo nitaeleza baadhi ya haki za mfanyakazi.

1. HAKI YA KUJUA SEHEMU YA KUFANYIA KAZI.

Isiwe uliambiwa eneo la kazi ni Dar es salaam halafu ujikute kila siku una safari za mikoani halafu uambiwe eti hiyo ndiyo kazi yenyewe, hapana. Lazima eneo la kufanyia kazi lijulikane kwa mfanyakazi. Ijulikane kuwa umeajiriwa na eneo lako la kazi ni Dar es salam , au Mwanza au Kagera.

Hii ina maana kubwa kwakuwa mfanyakazi asipojua eneo lake la kazi hataweza kudai malipo yatokanayo na kufanya kazi nje ya ofisi . Lakini iwapo unajua eneo lako la kazi basi utakapokuwa nje ya eneo la kazi yakupasa kudai malipo ya ziada. Kwa hiyo hakikisha mwajiri wako unakuainishia kwa uwazi kabisa eneo lako la kazi na ulijue. Nje ya hilo eneo ni malipo mengine ambayo ni nje ya mshahara wa kawaida.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...